
Gari la Mhariri wa gazeti la Rai na Naibu Mhariri Mtendaji wa New Habari, Danny Mwakiteleko, Danny alipata ajali juzi usiku (jumatano) eneo la Tabata (ToT) na kukimbizwa katika Hospitali ya Amana, Ilala na baadaye Muhimbili.Katika ajali hiyo gari alilokuwa akiendesha Danny liligongwa na lori lenye trela, ambalo lilitoweka bila kujulik...ana saa nne usiku. Mwakiteleko alikuwa akitokea kazini Sinza ambako alifanya kazi hadi saa tatu usiku.Danny alipelekwa katika Hospitali ya Amana kwa uangalizi hadi saa 12 asubuhi, ambapo madaktari waliamua apelekwe Hospitali ya Taifa Muhimbili.Baada ya uchunguzi Muhimbili, madaktari walisema majeruhi alikuwa ameumia kichwani na kumfanya apoteze fahamu kiasi (semi-conscious) hivyo ikabidi apelekwe katika chumba cha upasuaji ambako madaktari walimhangaikia kuanzia saa sita hadi saa tisa mchana. Na hatimae Danny amefariki dunia. Mwenyeenzi Mungu amemhitaji mja wake